Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (as) -ABNA-: Mkusanyiko huo ulifanyika kwa ushiriki wa idadi ya watu wa Venezuela, ambapo washiriki walionyesha mshikamano wao na watu wa Palestina kwa kushikilia mabango na kutoa hotuba mbalimbali za kuisapoti Gaza na Palestina kwa ujumla.
Wandau wa mkutano huo walilaani vikali mauaji ya halaiki yanayoendelea Palestina, na kwa nguvu walipinga sera na vitisho vya serikali ya Donald Trump kuhusu uwezekano wa kuingilia siasa za Venezuela.
Washiriki walisisitiza kuwa maandamano na shughuli za uungaji mkono wa watu wa Palestina yataendelea mitaani, na wakabainisha thamani za kibinadamu pamoja na mshikamano wa wananchi wa Venezuela.
Tukio hili ni sehemu ya jitihada za kudumu za watu wa Venezuela kuongeza uelewa juu ya hali mbaya ya Gaza na kulinda haki za mataifa pamoja na uhuru wa taifa lao.
Your Comment